RWANDA NA TANZANIA ZANUIA KUSHIRIKIANA KATIKA SEKTA YA MAZIWA
Zanzibar. Mnamo tarehe 12 Januari 2024, Serikali za Rwanda na Tanzania ziliingia makubaliano ya kushirikiana kuendeleza Sekta ya Maziwa (Dairy Industry). Waliotia saini katika Hati ya Makubaliano ni Waziri wa Nchi anayeshughulikia Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kikanda wa Rwanda, Mhe Jenerali (Rtd) James Kabarebe, na Waziri wa Mifugo na Uvuvi wa Tanzania Mhe. Abdallah Ulega (Mb).

Hafla hiyo ilishuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Mhe. January Makamba, Naibu wake Mhe. Stephen Byabato na viongozi wengine kutoka wizara hiyo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Bodi ya Maziwa Tanzania.
Wengine ni Balozi wa Rwanda nchini Tanzania Mhe. Fatou Harerimana na Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Mhe. Maj. Jen Ramson Godwin Mwaisaka.
Rwanda inajizatiti kama moja ya wazalishaji wakuu wa tungsten duniani, ikiwa ya 7 duniani na ya kwanza barani Afrika. Mafanikio haya yanatokana na Mgo…
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Jamhuri ya Rwanda…
Rais Samia Suluhu Hassan wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiagana na Balozi wa Rwanda Nchini Tanzania Mhe. Fatou Harerimana mara baada ya…
On 13th May, 2024, Rwanda High Commission in Tanzania administered an oath, and issued a Certificate of Rwandan Nationality, to Ms. Anoek De Smet, a…