MAADHIMISHO YA NNE YA SIKU YA LUGHA YA KISWAHILI DUNIANI YAFANYIKA NCHINI RWANDA
Serikali ya Rwanda, kupitia Wizara ya Elimu, iliandaa Maadhimisho ya Nne ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika kwa siku mbili (6-7 Julai 2025), ikiwakutanisha washiriki zaidi ya 300—wakiwemo viongozi waandamizi wa serikali, wasomi, vijana, na wataalamu wa Kiswahili—kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki na maeneo mengine.

Maadhimisho hayo yalikuwa chini ya KauliMbiu “Kiswahili, Elimu Jumuishi na Maendeleo Endelevu,” yakiambatana na hafla ya ufunguzi ya ngazi ya juu, kongamano la kikanda, jukwaa la vijana, pamoja na maonesho ya umma. Kila shughuli ilisisitiza imani ya pamoja kwamba Kiswahili ni zaidi ya lugha—ni chombo chenye nguvu cha umoja, utambulisho, na maendeleo.
Akihitimisha maadhimisho hayo, Waziri wa Nchi (Elimu) Bi. Claudette Irere alizungumzia kuhusu dhamira ya kimkakati ya Rwanda katika kukuza Kiswahili. Alikumbusha kwamba mnamo mwaka 2017, Rwanda ilitangaza rasmi Kiswahili kuwa mojawapo ya lugha zake za taifa—si kama ishara tu, bali kama hatua ya makusudi ya kuimarisha ujumuishi wa kikanda na nafasi ya Rwanda katika mandhari pana ya lugha na utamaduni wa Afrika.

Pichani: Bi Claudette Irere
“Kiswahili kina jukumu muhimu katika kukuza elimu jumuishi na yenye usawa,” alisema. “Uamuzi wetu uliongozwa na maono ya kuimarisha mahusiano ya kitamaduni, ushirikiano wa kikanda, na mshikamano wa Afrika.”
Aidha, Waziri alieleza maendeleo ambayo Rwanda imepiga katika kukuza Kiswahili kupitia mfumo wake wa elimu—kuanzia kufanya Kiswahili kuwa somo la lazima katika shule za sekondari ya chini, hadi kuwekeza katika mafunzo ya walimu na kusaidia tafiti za Kiswahili katika elimu ya juu.
Kadri maadhimisho yalivyokamilika, ujumbe mmoja ulijitokeza kwa nguvu: Rwanda inaona Kiswahili si tu kama lugha ya kufundishia, bali kama kichocheo cha umoja, ubunifu na ujumuishi wa Afrika.



Rwanda inajizatiti kama moja ya wazalishaji wakuu wa tungsten duniani, ikiwa ya 7 duniani na ya kwanza barani Afrika. Mafanikio haya yanatokana na Mgo…
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Jamhuri ya Rwanda…
Rais Samia Suluhu Hassan wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiagana na Balozi wa Rwanda Nchini Tanzania Mhe. Fatou Harerimana mara baada ya…
On 13th May, 2024, Rwanda High Commission in Tanzania administered an oath, and issued a Certificate of Rwandan Nationality, to Ms. Anoek De Smet, a…